Header Ads

Breaking News

Vigogo wa upinzani matatani Washinikizwa kurejesha kadi za CCM

Vigogo  wa upinzani matatani
 Washinikizwa kurejesha kadi za CCM

TAKRIBAN viongozi wote wa kitaifa kambi ya upinzani wameanza kutafuta njia ya kujinusuru ili kuthibitisha ukweli wao baada ya Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani kuthibitisha bado ni mwanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili tangu Katibu Mwenezi wa CCM Bw. Nape Nnauye aeleze kwamba mwenzake wa CHADEMA Dk. Wilbrod Peter Slaa ni mnafiki anabeba kadi ya vyama viwili vya siasa vigogo kadha wameanza kukutana kupanga mikakati ya kujieleza wakiibuliwa.
Dk. Slaa hakupenda kupoteza muda wa jamii kukanusha bali aliripotiwa kukiri uanachama wa CCM, lakini anasema kadi hiyo ameamua kubaki nayo kama kumbukumbu yake.
Ameshindwa kusimamia ushahidi wake anaotoa kila mara kutaka wanachama wa CCM wapeleke kadi zao CHADEMA wanapoamua kukimbilia upinzani badala ya kudhihirisha walikozipata au kubaki nao kama alivyofanya.
Kiwewe hiki pia kimezingira majaliwa ya Mwenyekiti wa TLP Bw. Agustine Lyatonga Mrema ambaye naye aliwahi kukiri miaka 12 iliyopita kwenye kipindi cha Kitimoto kwamba anayo kadi ya CCM yaani hajakana ukereketwa kwa vitendo.
Kwa mtiririko huo Bw. Mrema ni mwanachama wa vyama vitatu vya siasa ambayo ni CCM, NCCR-Mageuzi na sasa TLP ambako huko ni Mwenyekiti.
Hakuna kumbukumbu rasmi za kuonyesha kwamba Profesa Ibrahim Haruna Lipumba wa CUF aliwahi kurudisha kadi ya CCM alipoacha kazi mwaka1994 kumshauri Rais na kukimbilia mrengo wa kushoto.
Ungamo la Dk. Slaa litamuweka pabaya Profesa Lipumba na Maalim Seif Sharif amekuwa mstari wa mbele kuikaba serikali ya CCM wakati naye ni mmoja wa wafuasi wa chama hicho.
Huko NCCR-Mageuzi, UPDP,SAU,TADEA, ADC naUDP vikao vya siri vinaendelea kuzima azma ya Bw. Nape kuwafichua wanaojidai mitaani usiku kwa kutumia kadi za CCM lakini mchana huibuka na kujifanya ni vinara wa kutetea wanyonge kwa majoho ya upinzani.
Bwana James Mbatia wa NCCR-Mageuzi, John Momose Cheyo (UDP), Fahmi Dovutwa (UPDP) Paul Kyara (SAU) Saidi Miraji (ADC) na John Chipaka wa TADEA wanajulikana kuwa hawajachoma mbeleko ya CCM bali wanajipa moyo kubaki upande usiokuwa na tija. 
Katika mahojiano na wanasiasa kadha idadi kubwa wamemtaka msajili wa vyama vya siasa atoe ufafanuzi kuhusu watu wenye kadi za vyama vya siasa zaidi ya kimoja hasa inapotokea mtu anagombea urais, ubunge na udiwani.
Kundi jingine limesema huo ni unafiki mtu mzima kukosa uamuzi wa kujua chama anachofuata hivyo wale vigogo wanaobainika wachague moja kubaki upinzani au warudi walikotoka.
Jeuri ya viongozi wa CHADEMA kudandia hoja na kupindisha ukweli imeota mbawa lilipojitokeza suala la Katibu Mkuu wao kuthibitisha anatii kanuni za vyama viwili CCM na CHADEMA ambayo haviwezi kukaa meza moja kwa hali yoyote.

No comments