Ebola:Raia wa S Leone kusalia majumbani
Takriban watu millioni sita wametakiwa kusalia majumbani mwao kwa kipindi cha siku tatu huku watu wa kujitolea wakitembelea nyumba hadi nyumba kuwasaka watu walio na ishara za ugonjwa huo huku wakiwashauri wengine jinsi ya kuepuka maambukizi.
Visa kadhaa bado vinaendelea kuripotiwa kazkazini na Magharibi mwa Sierra Leone kila wiki.
Mataifa matatu ya Afrika Magharibi yalioathiriwa vibaya na Ebola Sierra Leone,Liberia,Guinea-yameweka lengo la kutokuwa na hata kisa kimoja cha ebola ifikiapo katikati ya mwezi ujao.
No comments
Post a Comment